ZAIDI YA SHILINGI BILIONI 1.3 ZA MADAI YA WALIMU MKOANI KATAVI HAWAJANUSA


Chama Cha walimu Tanzania CWT Mkoani Katavi kimesema madai mbalimbali ambayo walimu wanaidai serikali mpaka sasa hayajalipwa.
Hatua hiyo imethibitishwa na Katibu wa chama hicho Mkoani Katavi Hamis Ismail Chinahova wakati akizungumzia kuhusu hatua iliyofikiwa ya kulipwa kwa madeni ya walimu.
Aidha amesema kiasi cha cha shilingi bilioni 1.3 ambacho walimu Mkoani Katavi wanaidai serikali kinahusu madai ya likizo,uhamisho,matibabu,masomo na stahiki nyingine muhimu ukiondoa suala la mishahara.
Kwa mjibu wa taarifa ya iliyokuwa imetolewa na Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango hivi karibuni,takwimu ya madeni ya watumishi nchini inaonesha ni  zaidi ya shilingi bilioni 127 kati ya hizo walimu wakidai shilingi bilioni 16.25 zilizotakiwa kulipwa pamoja na mshahara wa mwezi Februari mwaka huu.

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA