WATOTO PASUA VICHWA SUMBAWANGA


BARAZA la madiwani la halmashauri ya Manispaa ya Sumbawanga mkoani Rukwa limeviomba vyombo vya usalama vishirikiane na idara ya uhamiaji  kuwakamata na kuwarudisha nchini kwao watoto wa nchi jirani za Zambia na  Congo DRC wanaoishi katika mazingira magumu.
Mstahiki Meya wa Manispaa ya Sumbawanga Justine Malisawa alitoa kauli hiyo hivi karibuni wakati akiongoza kikao cha baraza hilo baada ya wajumbe kulalamikia kuongezeka kwa watoto ambao wamekuwa kero na kujihusisha vitendo vya uporaji wa mali za raia pamoja na ubakaji.
Mmoja wa madiwani hao Vitalis Ulaya alisema watoto hao wanazidi kuongezeka kila kukicha katika mji wa Sumbawanga hali ambayo ni hatari kwa kuwa hakuna jitihada za kutosha za kuweza kukabiliana na wimbi la ongezeko hilo.
Alisema kuwa wengi wa watoto hao wanazurula nyakati za mchana  wakiokota vitu majalalani na kuomba hela kwa wapita njia na nyakati za usiku wamekuwa wakifanya vitendo vya uhalifu hali inayosababisha amani kutoweka.
Kwa upande wake Ester Mpelele mjumbe wa baraza hilo alisema watoto hao wamekuwa ni changamoto kubwa kwa wanawake kwani hivi sasa hawawezi kutembea peke yao nyakati za jioni na usiku hali ambayo aliiomba serikali kuingilia kati jambo hilo.
Aliwaomba wazazi katika Manispaa hiyo ya Sumbawanga kuwajibika katika malezi ya watoto wao kwani kitendo cha kuwaacha bila kuwapa huduma za msingi ikiwemo elimu wanawaandalia maisha mabaya ya baadaye na watakuja kuisumbua jamii kutokana na kushindwa kuwajibika kwao.

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA