WANANCHI WALALAMIKIA UONEVU KATAVI


Wananchi wa kitongoji cha Itogolo katika kijiji cha Kampuni  kata ya misunkumilo Halmashauri ya Manispaa ya Mpanda Mkoani Katavi,wameilalamikia serikali kuwakamata,kuwatoza faini na kuwalazimisha kuvuna mazao yao kabla ya kukomaa.
Wananchi hao wakiwemo Agnes John,Charles Pius na Peter Luamula wametoa malalamiko hayo katika mkutano wa hadhara wa kijiji cha Kampuni ambapo ulikuwa ukifanyika katika kitongoji hicho lengo likiwa ni kutoa nafasi kwa wananachi kueleza kero zao.
Wamesema wamekuwa wakikamatwa ovyo na mgambo kisha kupelekwa mahabusu na kulipishwa faini wakati hakuna elimu ya kutambua mita sitini kutoka chanzo cha maji ya mto Mpanda iliyotolewa.
Kwa upande wao wajumbe wa kamati ya watumia maji bonde la mto Mpanda Mahela Mahanda na Daudi Sumuni wamekanusha kuwaamrisha wananchi kuvuna mazao yao kabla ya kukomaa lakini wamekubali kuwakamata na kuwatoza faini kabla ya kutoa elimu kwa wananchi hao.
Mwenyekiti wa kijiji cha Kampuni Bw.James Simoni amesema mpaka sasa watu watatu wamekamatwa na kutozwa faini katika kitongoji hicho chenye kaya zipatazo 71 zinazotegemea mto Mpanda kuendesha maisha yao.
Hata hivyo naye amekiri kuwa elimu katika kitongoji hicho ilikuwa haijatolewa lakini amesema wananchi hao walikuwa na taarifa tangu mwaka jana.
Habari kamulu ni WWW.P5TANZANIA.BLOGSPOT.COM  

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA