DKT.SHEIN AWAAPISHA MAKATIBU WAKUU


RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein,leo amewaapisha viongozi aliowateua hivi karibuni kushika nyadhifa mbalimbali katika Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.
Viongozi walioapishwa na Rais Dk.Shein katika hafla iliyofanyika Ikulu Mjini Zanzibar ni Fatma Gharib Bilal ambaye ameapishwa kuwa Katibu Mkuu Wizara ya Kazi,Uwezeshaji,Wazee, Wanawake na Watoto na Abdalla Hassan Mitawi ambaye ameapishwa kuwa Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Makamo wa Pili wa Rais.
Hafla hiyo ilihudhuriwa na viongozi mbalimbali akiwemo Makamu wa Pili wa Rais Balozi Seif Ali Idd,Spika wa Baraza la Wawakilishi Zubeir Ali Maulid,Jaji Mkuu wa Zanzibar  Omar Othman Makungu,Mwanasheria Mkuu wa Zanzibar Said Hassan Said pamoja na Mawaziri.
Viongozi wengine waliohudhuria hafla hiyo ni Mufti Mkuu wa Zanzibar Sheikh Saleh Omar Kabih,Kadhi Mkuu wa Zanzibar Sheikh Khamis Haji,Mkuu wa  Mkoa wa Mjini Magharibi Ayoub Mohamed Mahmoud,Washauri wa Rais wa Zanzibar pamoja na viongozi wengine wa Serikali.
Kwa upande wa walioapishwa waliahidi kutekeleza majukumu yao kwa ushirikiano wa pamoja kati yao na viongozi wengine wote wa Serikali wakiwemo wale wa Wizara zao pamoja na Ofisi watakazoziongoza.
Habari zaidi ni WWW.P5TANZANIA.BLOGSPOT.COM

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA