ZANZIBAR KUADHIMISHA SIKU YA SHERIA



Jaji mkuu wa Zanzibar Omar Othman Makungu amesema katika kuadhimisha siku ya sheria Nchini ,mahakama imekusudia kuandaa maonesho maalumu kwa ajili ya kutoa elimu ya sheria kwa wananchi ili kupunguza uvunjifu wa sheria.
 Akizungumza na waandishi wa Habari kuhusiana na shamrashamra za siku ya Sheria Jaji makungu amesema maonesho hayo yatakayodumu kwa muda wa siku tatu pia yatawapa fursa wafanya bishara kuuza biashara zao.
Amesema mbali na Maonesho hayo pia  Kutakuwa na Ufunguzi wa Mahakama ya Wilaya ya mwanakwerekwe baada ya kumalizika kwa ukarabati wa Mahakama hiyo ambayo itafunguliwa na Raisi wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Muhammed Shein.
 Aidha amesema katika shamrashamra hiyo kutakuwa na matembezi ya siku ya sheria yatayoongozwa na Spika wa baraza la wawakilishi kwa lengo la kuhamasisha wananchi kujua umuhimu wa kufuata sheria.
Akizungumzia mafanikio waliyapata katika uendeshaji wa kesi kwa wananchi hususan kesi za Udhalilishaji amesema mpaka sasa usimamizi wa kesi unakwenda vizuri jambo ambalo linapelekea wananchi kunufaika na haki zako za msingi licha ya kuwepo kwa mapungufu katika masuala ya ushahidi.
Amesema wananchi wamekuwa na mwamko wa kuripoti kesi hizo lakini zinashindwa kuendelea kutokana na wananchi kushindwa kuleta ushahidi kwa wakati na kusababisha ugumu katika utoaji wa maamuzi.
Akijibu maswali ya waandishi wa habari kuhusiana na uingizwaji na Usambazaji wa dawa za kulevya jaji Makungu amesema bado kuna ugumu katika uendeshaji wa kesi za madawa ya kulevya kutokana kesi nyingi hazijapatiwa hukumu kwa kukosekana kwa ushadi.
Siku ya sheria nchini huadhimishwa kila ifikapo Feb12 ya kila mwaka ambapo kwa Zanzibar itaadhimishwa katika Ukumbi wa Barza la wawakilishi la Zamani Mjini unguja na kauli mbiu ya mwaka huu ni  ‘’kuimarisha utawala wa sheria kwa kukuza Uchumi wa Nchi’’.
Habari zaidi ni P5TANZANIA LIMITED

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA