ANC CHAZIDISHA SHINIKIZO DHIDI YA ZUMA MGUU SAWA KATIKA MKUTANO WA KESHO



Chama tawala nchini Afrika Kusini ANC kimeitisha mkutano wa viongozi wake wa juu utakaofanyika kesho huku kukiwa na taarifa kwamba mkutano huo ni kwa ajili ya kujadili shinikizo la kumtaka rais Jacob Zuma kuachia madaraka.
Rais Jacob Zuma atakiwa kujiuzuru
Hata hivyo kauli ya chama cha ANC iliyotolewa kuhusiana na mkutano huo imesema,wanakutana kujadili ubadilishanaji madaraka kutoka Rais Zuma kama mwenyekiti wa zamani na sasa Cyril Ramaphosa ambaye ni kiongozi mpya wa chama hicho.
Siku ya jumatatu viongozi wandamizi wa chama hicho walilazimika kuwa na mkutano wa dharula mjini Johannesburg kujadili hatima ya rais Zuma.
Kwa upande wake rais Zuma ameshikilia msimamo wake kutokubaliana na shinikizo la kumtaka aachie madaraka.
Mwezi Disemba mwaka jana Ramaphosa alimrithi rais Zuma katika nafasi ya juu ya kukiongoza chama hicho kikongwe barani Afrika.
Nafasi ya urais ya Zuma imekuwa ikiandamwa na kashfa za rushwa, ambapo katika miaka ya hivi karibuni alihusishwa na familia yenye asili ya India ijulikanayo kama Gupta ambapo inadaiwa alitumia madaraka yake vibaya ili kujinufaisha yeye na washirika wake hao.
Habari zaidi ni P5TANZANIA LIMITED

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA