SERIKALI YAOMBWA KUWAANGALIA UPYA WATU WENYE ULEMAVU ZANZIBAR



Mkurugenzi  Umoja wa watu wenye ulemavu Zanzibar Asia Abuu Salami  ameiomba serikali  na Taasisi mbalimbali za maendeleo nchini,kuwapa kipaumbele zaidi watu wenye ulemavu na wasiojiweza pindi zinapotokea   fursa za kimaendeleo kwa wananchi.
Amesema  ni vyema Watu wenye ulemavu  kupewa haki sawa za kimaendeleo na watu wengine wasokuwa na ulemavu ili kila mmoja wao ajihisi huru kama wengine kwani nao wakiwezeshwa wanaweza.
Aidha Mkurugenzi  Asia  amebainisha kuwa  bado watu wenye ulemavu  wanakabiliwa na changamoto  nyingi katika jamiii ikiwemo ukosefu wa vifaa wanavyotumia kwa shughuli zao za kila siku kama vigari vya kutembelea,Fimbo,Miwani na kadhalika.
Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Kusini Unguja Mhe Hassan Hatibu Hassan amewashauri watu wenye ulemavu  Mkoani humo kuanzisha Jumuiya  ya pamoja itakayowawezesha kurahisisha upatikanaji wa mahitaji yao.
Habari zaidi ni P5TANZANIA LIMITED

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA