RAIS ASEMA ATAJUA ATAKAVYOFANYA WATAKAOBORONGA MAHAKAMANI, AWABADILIKIA MWANASHERIA MKUU WA SERIKALI PIA WAZIRI WA SHERIA





Rais wa Tanzania Dkt.John Magufuli alisema bado kuna tatizo kubwa katika ofisi ya DPP (Mkurugenzi wa Mashtaka) na AG (Mwanasheria Mkuu),na ndiyo maana muda mwingine inawapelekea kuwapa changamoto kubwa Majaji.
Kwa upande mwingine,Rais Magufuli amewataka viongozi wengine wanaosimamia vyombo vya sheria kufuata mfano mzuri aliyouanzisha Profesa Ibrahimu Juma kwa kutowafumbia macho wahalifu wa aina yeyote ile.
Rais ambaye alikuwa mgeni rasmi katika shughuli hizo aliongozana viongozi wengine wa serikali.
Wakti huo huo Rais  Dkt.Magufuli leo amewabadilikia Waziri wa Katiba na Sheria,Prof.Palamagamba Kabudi na Mwanasheria Mkuu wa serikali,George Masaju na kudai kuwa wanakwamisha haki kutendeka kwa watu kutokana na kutofanyia kazi mambo ya msingi.
Amesema yeye ameumbwa kusema ukweli hivyo ataendelea kuusema hata kama kuna watu unawaumiza.
Wakati huo huo Rais Magufuli kupitia kilele cha maadhimisho ya 22 ya siku ya Sheria amewapa pole Majaji kwa changamoto wanazokumbana nazo pindi wanaposhughulikia mashitaka yanayopelekwa na serikali na kuahidi kulifanyia kazi jambo hilo kabla ya mwezi Februari kuisha huku akidai ameshajifunza vya kutosha.
Habari zaidi ni P5TANZANIA LIMITED

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA