SERIKALI KUTATUA KERO YA MAJI VIJIJI VYA JIMBO LA KAVUU


Wizara ya maliasili na utalii inatarajia kutatua kero ya maji kwa wakazi wa kata ya Itobanilo na vijiji vyake katika Halmashauri ya Wilaya ya Mpimbwe Mkoani Katavi,ili kuondoa mgogoro kati ya askari wa wanayama pori na wananchi wanaotegemea maji ya mto Kavuu uliopo hifadhi ya taifa ya wanyama ya Katavi.
Kauli hiyo imetolewa na Naibu waziri wa zira hiyo Mh.Josephat Hasunga,wakati akijibu swali la  Mbunge wa Jimbo la Kavuu Mh.Pudensiana Kikwembe aliyetaka kujua kauli ya serikali kuhusu askari wa wanyama pori wanaowanyanyasa wananchi wanaopata huduma ya maji katika mto Kavuu.
Akijibu swali hilo,Mh.Hasunga amesema wizara kwa kushirikiana na mbunge pamoja na wananchi watajadili kwa pamoja ili kutatua kero ya maji ambapo kwa sasa wananchi wanahatarisha afya zao kwa kuchota maji katika hifadhi na kukiuka sheria za nchi.
Mbali na Vijiji vya Sentaunyenye,Senta Amani na Lunguya katika halmashauri ya Wilaya ya Mpimbwe kutegemea maji kutoka maeneo ya hifadhi pia wakazi wa kata ya sitalike Halmashauri ya wilaya ya Nsimbo nao wamekuwa wakitegemea maji kutoka mto Katuma ambao ni sehemu ya hifadhi.
Habari zaidi ni P5TANZANIA LIMITED


Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA