WANAWAKE WAJAWAZITO WILAYANI MPANDA WANALAZIMIKA KUBEBA MAJI KUTOKA NYUMBANI MPAKA ZAHANATI KWA AJILI YA USAFI WAKATI WA KUJIFUNGUA

Na.Issack Gerald
Wanawake wote wajawazito katika kijiji cha Mtambo kata ya Katumba Halmashauri ya wilaya ya Nsimbo Mkoani Katavi, wanalazimika kubeba maji kutoka nyumbani na kuyapeleka katika zahanati ya Mtambo iliyopo kijijini hapo ili yatumike wakati wakijifungua.
Mganga mfawidhi wa zahanti hiyo Dkt.Daud Mashama amesema wanawake wajawazito wasipokuja na maji hulazimika kufuata maji mto Kalutonya uliopo umbali wa kilomita 8 kutoka zahanati ya Mtambo.
Kaimu afisa Mtendaji wa kata ya Katumba Bi.Lucy Kagine amekiri kuwepo kwa tatizo la maji katika kijiji cha Mtambo huku akisema mara kwa mara kila wanapochimba visima upatikanaji wa maji umekuwa mgumu.
Kwa upande wake Katibu wa kijiji cha Mtambo Bw.Fenias Fulujensi pamoja na mambo mengine amesema wanasubiri uwekaji wa mitambo katika kisima kilichochimbwa ili kusukuma maji.
Kwa mjibu wa wakazi wa kijiji cha Mtambo,zahanati ya Mtambo ilijengwa miaka ya 1992 ambapo hata hivyo Juhudi za kutafuta uongozi wa Halmashauri ya wilaya ya Nsimbo kuhusiana na tatizo hilo zinaendelea.
Hivi karibuni wakazi wa Kata ya Katumba walilalamika kukosa maji ya chanzo cha maji ya Ikorongo wakisema maji kusafirishwa kutoka kata ya Katumba mpaka Mpanda Mjini na wao kukosa huduma hiyo licha ya chanzo hicho kuwa katika kata yao serikali haiwatendei haki.
Serikali ya awamu ya tano chini ya uongozi wa Rais John pombe Magufuli inajinasibu kuwa moja kati ya mipango iliyopo katika ilani ya CCM ya mwaka 2015-2020 inasema inalenga kumtua mama ndoo kichwani ambapo kwa mjibu wa hali iliyopo katika kata ya Katumba bado ndoo inamlemea mama kichwani.

Habari zaidi ni P5TANZANIA LIMITED

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA