IGP SIRRO AWAOMBA VIONGOZI WA DINI MKOANI RUKWA KUHUBIRI AMANI ILI UHARIFU UPUNGUE

Na.Issack Gerald
Mkuu wa jeshi la polisi nchini IGP Simon amewaomba viongozi wa dini mkoani Rukwa Kuongeza bidii katika kuhubiri amani ili mauaji yanayotokayo na imani za kishirikina na mapenzi yapungue mkoani humo. 
IGP Sirro ametoa kauli hiyo wakati akijibu maswali ya waandishi wa habari waliotaka kujua mikakati ya jeshi hilo katika kukabiliana na mauaji mkoani humo.
Amesema jeshi la polisi linajitahidi kukabiliana na mauaji yote yanayotokea nchini lakini katika Mkoa wa Rukwa takwimu zinaonesha kuwa mauaji yanayotokana na ushirikina pamoja na  wivu wa mapenzi yanaongoza mkoani humo.
Kamanda Sirro amesema viongozi wa dini wana jukumu kubwa kuhakikisha wanahubiri amani ili mauaji hayo yapungue kwani juhudi hizo zinapaswa kuwa za pamoja kwa kuwa nao wana nafasi kubwa la kuwalea wananchi kiroho.
Wakati huo huo IGP Sirro ameahidi kuwa Jeshi hilo kupitia bajeti zake litajenga kituo kipya cha polisi cha Sumbawanga mjini kwa kuwa kilichopo ni kichakavu na majengo yanayotumika yalirithiwa kutoka kwa wakoloni.
Pamoja na kuahidi ujenzi wa kituo hicho,pia ameahidi kuupatia mkoa wa Rukwa gari moja jipya aina ya Lori litakalosaidia kutumika katika matumizi mbalimbali ya polisi mkoani humo kwa kuwa kuna upungufu wa vitendea kazi. 
Hata hivyo amewataka wananchi mkoani humo Kushirikiana na jeshi la polisi na kubadirika kuacha kubweteka kwani hivi sasa maisha yamekuwa tofauti na matukio mbalimbali yamekuwa yakiongezeka ni jukumu lao kujijali na kujiepusha kutofanya uhalifu. 
Kwa upande wake Mwenyekiti kamati ya wa ulinzi na usalama mkoani Rukwa Joachim Wangabo ambaye pia ni mkuu wa mkoa huo amemwambia IGP kuwa atajitahidi kuwashirikisha wafanyabiashara mkoani humo ili wajenge nyumba za kuishi polisi kwa kuwa hawawezi kusubiri mpaka serikali ifanye kazi hiyo. 

Habari zaidi ni P5TANZANIA LIMITED

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA