HALMASHAURI YA WILAYA YA NSIMBO YAKABIDHI MSAADA WA BAISKELI 20 ZENYE THAMANI YA MILIONI 11 KWA WATU WENYE ULEMAVU

Na.Issack Gerald-Nsimbo Katavi
HALMASHAURI ya Wilaya ya Nsimbo Mkoani Katavi,imekabidhi msaada wa baiskeli ishirini za tairi tatu zenye thamani ya shilingi milioni kumi na moja kwa watu wenye ulemavu katika halmashauri hiyo.

Akikabidhi msaada huo kaimu mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo Bw.Frednandi  Filimbi pamoja na mambo mengine ameitaka jamii kutowaficha watu wenye ulemavu ili wapate haki zao stahiki.
Aidha Bw.Filimbi amesema kwa sasa Halmshauri inatafuta fedha ili kujenga bweni katika mojawapo ya shule itakayochaguliwa ndani ya Halmshauri ili kuwajengea mazingira ya watoto kusoma wakitokea katika eneo moja.
Kwa upande wake Afisa ustawi wa Jamii Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo Bi.Dianarose Mnuo,ameonya watu wasiohusika wakiwemo watu wakubwa na watoto kuchezea baiskeli ambazo zimetolewa maalumu kwa watu wenye ulemavu.
Mwakilishi wa kampuni ya uwindaji wanyama hapa nchini Conservation Foundation Tanzania (CFT) Bi.Rose Beker ambao ndiyo wamekabidhi msaada huo kwa Halmashauri ya Nsimbo,amesema wataendelea kutoa msaada katika maeneo mbalimbali Mkoani Katavi.
Kwa mjibu wa Afisa elimu Maalumu Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo Clevery Mngao,Halmashauri watu wenye ulemavu 105 waliokwishawabaini wanaohitaji kupata msaada.
Nao baadhi ya wanuafaika wa msaada huo akiwemo Elias Michael ambaye ni mwanafunzi wa darasa la tatu katika shule ya Msingi  Mtambo amesema baiskeli hiyo itamsaidia kumrahishia safari wakati wa kwenda shule huku wazazi na wakiomba makampuni mengine kuiga mfano wa kampuni hiyo kwa kutoa msaada zaidi kwa makundi maalumu.
Watu hao wenye ulemavu waliokuwa mchanganyiko wa watoto,wazee,vijana wanawake kwa wanaume wanatoka katika maeneo kata mbalimbali za Halmshauri ya Wilaya Nsimbo.
Watu hao 20 waliopatiwa msaada ni miongoni mwa watu wenye ulemavu 49 ambao Halmashauri ilikuwa imewaombea msaada.
Habari zaidi ni www.p5tanzania.blogspot.com au ukurasa P5Tanzania Limited au P5Tanzania Limited


Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA