BREAKING NEWS: RAIS MAGUFULI AFANYA MABADILIKO KATIKA BARAZA LA MAWAZIRI,ATEUA PIA MAWAZIRI

Rais Dkt John Magufuli wa Tanzania
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.John Pombe Magufuli,amefanya mabadiliko ya Baraza la Mawaziri.

Tukio hilo limetokea leo ambapo Rais Magufuli pia amezigawa Wizara ya Kilimo,Mifugo,Uvuvi na kuwa wizara ya Kilimo pekee na Wizara ya Mifugo na Uvuvi peke yake,huku Wizara ya Nishati na Madini ikigawanya na kuwa wizara mbili tofauti.
Sambaba na hilo pia Rais Magufuli amemteua Mh. George Haruna Mkuchika kuwa Waziri Ofisi ya Rais Utawala Bora,ambaye kabla ya kuteuliwa alikuwa Mwenyekiti wa Kamati ya Haki,Maadili na Madaraka ya Bunge.
Kwa mabadiliko hayo wizara zimeongezeka kutoka 19 zilizokuwepo na hivyo kufikia wizara 21.
Mawaziri hao wanatarajiwa kuapishwa siku ya jumatatu Oktoba 9,Ikulu jijini Dar es salaam.

Habari zaidi ni www.p5tanzania.blogspot.com au ukurasa P5Tanzania Limited au P5Tanzania Limited Group 

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA