WAKUU WA MIKOA 10 AKIWEMO WA KATAVI WAAGIZWA KUSIMAMIA ZAO LA KILIMO-Septemba 10,2017

Waziri Mkuu,Kassim Majaliwa amewaagiza wakuu wa mikoa 10 inayolima pamba nchini akiwemo mkuu wa mkoa wa Katavi,kusimamia zao hilo kwa karibu ili kuinua uzalishaji wake na kuwaongezea kipato wananchi.

Majaliwa ametoa agizo hilo jana wakati akizungumza na wakuu hao wa mikoa,katika kikao alichokitiisha mjini Dodoma ili kujadili mbinu za kufufua zao hilo.
Majaliwa amesema Serikali imeamua kusimamia kilimo cha pamba kuanzia maandalizi ya shamba,kupanda, matumizi ya pembejeo na dawa,kuvuna,kutafuta masoko ambapo amewataka wasimamie katika maeneo yao ili kilimo cha zao hilo kibadilike.
Wakulima wa pamba wamekuwa wakilalamikia bei kubwa ya pembejeo ambazo husambazwa na mawakala,huku wakipewa baada ya mavuno wakipewa bei ambayo hailingani na gharama za uzalishaji.
Wakulima wamekuwa wakilalamikia kuuziwa mbegu ambazo hazioti na hakuna fidia ambayo hulipwa.
Wakuu wa mikoa waliohudhuria kikao hicho ni kutoka Shinyanga,Singida,Kagera,Tabora,Morogoro,Mara, Mwanza,Simiyu,Katavi na Geita.

Habari zaidi ni www.p5tanzania.blogspot.com

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA