WAKAZI WILAYANI MLELE WATAKA MIFUGO IDHIBITIWE KULINDA MAZINGIRA-Julai 11,2017

WAKAZI wa mtaa wa Katandala kata ya Majimoto Mkoani Katavi,wameuomba uongozi kushughulikia uzururaji holela wa mifugo.

Wakizungumza na Mpanda Radio Fm,wakazi hao wamesema kuwa,wanyama wakiwemo nguruwe na mbuzi huzurura ovyo katika makazi ya watu na hivyo kupelekea uharibifu wa mazingira.

Aidha wameuomba uongozi kuhakikisha wanawapa zaidi elimu wananchi ili kuhakikisha wanajenga mazizi ya mifugo kuepuka migogoro isiyo ya lazima.

Kwa upande wake mwenyekiti wa kijiji cha Katandala Bw.Isaya Pausanda,amekili kuwepo kwa adha hiyo na amewataka wafugaji wote kuhakikisha wanafungia mifugo yao katika Mazizi.


Habarika zaidi na P5TANZANIA.BLOGSPOT.COM

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA