KATIBU TAWALA WILAYA YA MPANDA AWAAGIZA MADIWANI MANISPAA YA MPANDA KUWASHIRIKISHA WANANCHI KATIKA SHUGHULI ZA MAENDELEO NA TAARIFA ZAO ZA USHIRIKI ZIWEKWE WAZI-Julai 27,2017



KATIBU tawala Wilaya ya Mpanda Mkoani Katavi Bw.Sostenesi Mayoka,amewaagiza madiwani wa Halmshauri ya Manispaa ya Mpanda kuwashirikisha wananchi katika shughuli za maendeleo na kuonesha taarifa sahihi za ushiriki wao katika taarifa zinazoandaliwa.

Mayoka ametoa wito huo leo kwa niaba ya Mkuu wa Wilaya ya Mpanda kupitia kikao cha 4 cha mwisho wa mwaka cha Baraza la Madiwani cha Manispaa ya Mpanda ambacho kimefanyika Manispaa ya Mpanda .
Katika hatua nyingine Mkurugenzi mtendaji wa Manispaa ya Mpanda Bw.Michael Nzyungu,amesema hatua ya serikali kufuta ajira za watendaji wa kata na vijiji wasiokidhi vigezo vya ajira na wenye elimu ya kuanzia darasa la saba walioajiriwa kuanzia mwaka 2004,kumeathiri shughuli za maendeleo kwa kuwa shughuli mbalimbali zinazoendelea kufanyika zinakoswa usimamizi wa viongozi hao.
Mbunge wa Jimbo la Mpanda Mjini Mh.Sebastian Kapufi,kupitia kikao hicho,ameahidi kufuatilia vibali vya ajira kwa ajili Manispaa ya Mpanda ambapo Halmashauri nyingine hapa nchini zimeanza kupokea vibali vya ajira.
Kikao cha baraza kitaendelea kesho kwa ajili ya kujadili maendeleo ya Manispaa ya Mpanda baada ya leo kupokea taarifa mbalimbali za kata 15 za Manispaa.
Habari zaidi na P5TANZANIA.BLOGSPOT.COM

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA