VIJANA WATII AGIZO LA MKURUGENZI WA MANISPAA KUTOSAFISHA VYOMBO VYA USAFIRI KATIKA VYANZO VYA MAJI



Na.Issack Gerald Bathromeo-Mpanda
Vijana na watu waliokuwa wakitumia mto Mpanda eneo la daraja linalotenganisha Kata ya Mpanda Hotel na Misunkumilo kusafisha magari na vyombo vingine vya usafiri,wamesitisha shughuli hiyo kutii agizo la mkurugenzi wa Manispaa ya Mpanda akiwataka kutofanya shughul hiyo kwa lengo la kulinda vyanzo vya maji.

Baadhi ya vijana waliokuwa wakitegemea shughuli hiyo ya kusafisha magari,wakizungumza na Mpanda Radio,wamekiri kuondoka eneo hilo ambapo hata hivyo wamesema kuondoka kwao eneo hilo  kunawaahtiri kiuchumi kwa kuwa hawana vyanzo vingine vya mapato kuendesha familia zao.
Kwa upande wake Mwenyekiti wa Mtaa wa Misunkumilo Bw. Katabi Jonas,pamoja na mambo mengine ameiomba serikali ya Manispaa ya Mpanda kwa kushirkiana na serika;li ya Mtaa kuwasaidia vijana kutengeneza miradi ya maendeleo kwa kuwa kila eneo wanalofanya shughuli wanaondolewa kwa madai kuwa ni uvamizi wa maeneo.
Amesema kuwa watu zaidi ya 70 waliokuwa wakijipatia kipato  kutokana na shughuli ya kusafisha magari,pikipiki na vyombo vingine vya usafiri ambao wamepigwa marufuku,wengi wao ni vijana waliofukuzwa eneo la uchimbaji wa kokoto milima wa Kampuni kwa madai kuwa eneo linalochimbwa ni miliki ya Jeshi la Wananchi Tanzania(JWTZ)
Kwa mjibu wa Mwenyekiti wa mtaa wa Misunkumilo ambaye eneo eneo hilo lipo katika eneo lake,amesema kuwa katazo la kusafisha magari limekuwa likitolewa mara kwa mara amba-po mpaka  sasa ni takribani miaka 25.
Agizo la mwisho la Mkurugenzi kuwataka watu kutotumia mto Mpanda kusafisha magari na  vyombo vingine vya usafiri lilitolewa Ijumaa ya wiki iliyopita.
Hivi karibuni,miongoni mwa wakazi ambao wamekuwa walilalamika kuathiriwa na shughuli itokanayo na uoshwaji wa vyombo vya usafiri mto Mpanda ni pamoja na wakazi wa Kata ya Itenka Halmshauri ya Wilaya ya Nsimbo Wilayani Mpanda.
Habarika zaidi na P5TANZANIA.BLOGSPOT.COM

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA