WAFANYABIASHARA WAILALAMIKIA SERIKALI KUWAZUIA KUTEKELEZA HAPA KAZI TU,WANGOA MABANGO USIKU WA MANANE WAKIPINGA KUFUKUZWA ENEO LA KIBIASHARA



Na.Issack Gerald Bathromeo-Katavi
Wafanyabiashara wadogo waliopo genge la kufanyia biashara lililopo Mtaa na Kata ya Mpanda Hotel Manispaa ya Mpanda Mkoani Katavi wamelalamikia uongozi wa serikali ya Mtaa,kata ya Mpanda Hotel na Halmashauri ya Wilaya ya Mpanda kwa kutowapatia eneo maalumu la kufanyia biashara huku wakifukuzwa katika kila eneo wanalokwenda kufanyia biasahara.
Bango lililong'olewa na kutupwa kusikojulikana katika genge la biashara lililopo mtaa na kata ya Mpanda hotel lililopigwa marufuku(PICHA NA.Issack Gerald)
                                 


Wafanyabiasahara wadogo wakiwa katika genge wakiuza bidhaa zao katika genge lililopigwa marufuku(PICHA NA.Issack Gerald)
Genge jipya eneo la mtaa wa  Mpanda ana Kata ya Mpanda Hotel lililopigwa marufuku(PICHA NA.Issack Gerald)
                         

Wakizungumza kwa jazba na hasira katika genge hilo,wafanyabiasaha hao zaidi ya 300 sasa,wamesema kuwa wamechoshwa na usumbufu wanaoupata katika uongozi wa serikali hizo na wanachokitaka sasa ni kurudishiwa fedha yao au kupelekwa katika eneo lingine lililo karibu na makazi yao ambapo tofauti na hapo wataomba msaada zaidi ngazi zinazofuata.
Wamesema kuwa katika eneo ambalo walitimuliwa tangu Julai 24,viwanja wanavyouzia biashara hizo walipimiwa na kugawiwa kwa gharama ya shilingi 10,000/= kila mfanyabiashara ambapo hatua hiyo imewashangaza na kuwaumiza kuonekana kuwa hawana haki wakati viwanja hivyo walipewa na serikali ya mtaa na kata inayotambulika kisheria.
Mpaka sasa wamehamishwa na kufukuza katika maeneo matano kuanzia mwaka 2015 ambapo katika eneo la kwanza la karibu na machinjio ya Mpanda hotel walitimuliwa kwa madai kuwa watakanyagwa na ng’ombe na pia siyo eneo halali la soko.
Maeneo mengine waliyotimuliwa wafanyabiashra hao ni pembezoni mwa barabara iendayo Mkoani Kigoma kuanzia Mpanda na katika maeneo ya viwanja vya watu binafsi huku wanapotimuliwa ikiwa hakuna wanapooneshwa wanakotakiwa kupelekwa kufanya biashara zao katika mitaa yao.
Naye Mwenyekiti wa Mtaa huo Bw.Alfred Mtaita akitolea ufafanuzi wa suala hilo amesema,wananchi wapo eneo hilo kihalali kwa kuwa eneo hilo siyo mali ya Idara ya ujenzi Halmshauri ya Wilaya ya Mpanda wanaodai eneo hilo kuwa mali yao wakati ni  Chama cha Mapinduzi kata ya Mpanda Hotel.
Hata hivyo kwa upande wake Diwani wa Kata hiyo Mh.Willium Liwali ambaye naye anahusishwa na wafanyabiashara kuwaruhusu kutumia eneo hilo,amewataka kuendelea na biashara zao kama kawaida wakati mazungumzo ya kuleta suluhu yakifanyiwa kazi ili kuondoa mgogoro wa ummiliki halali kati ya Halmshauri ya Wilaya ya Mpanda na Chama cha Mapinduzi kata ya Mpanda Hoteli.
Wakati huo huo Siku ya Jumapili,mabango 3 kati ya 4 yaliyokuwa yamesimikwa katika viwanja hivyo yaling’olewa na kutupwa kusikojulina na watu wasiojulikana na hiyo ikiwa ni ishara ya wafanyabiashara hao kutokubaliana na aliyeweka bango hilo.
Jumla ya Shilingi miloni moja laki saba na na elfu hamsini (1,750,000/) zilikwishachangwa na wafanyabishara na kiasi cha fedha tayari kimetumika kujenga choo katika eneo hilo ambapo mgogoro huo umezuka rasmi tangu wiki iliyopita baada ya wafanyabiashara kuanza biashara zao.
Miongoni mwa bidhaa zinazouzwa katika genge hilo ni pamoja na mbogmboga,matunda,viazi na mitumba ya nguo.
Mapema mwaka huu,Waziri Mkuu wa Tanzania Mh.Kassim Majiliwa aliziagiza Halmshauri zote nchini kutenga maeneo ya uwekezaji.

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA