MIRADI 71 ILIZINDULIWA NA MWENGE WA UHURU MKOANI KATAVI



Na.Issack Gerald Bathromeo-Katavi
Jumla ya Miradi 71 ya maendeleo ilizinduliwa katika Mkoa wa Katavi huku baadhi ya miradi hiyo ikiwa katika sekta ya elimu,kupambana na rushwa,ujenzi wa Miundombinu ya barabara na afya.

Taarifa hiyo imetolewa na Mkuu wa Mkoa wa Katavi Meja Jenerali Mstaafu Raphael Mugoya Muhuga wakati akizungumza na waandishi wa habari Ofisini kwake.
Alisema kuwa katika miradi hiyo yote iliyokaguliwa na mwenge wa Uhuru ina thamani ya Shilingi Bilioni 16.3.
Aidha alitoa shukrani kwa wakazi wa Mkoa wa Katavi kwa kuonesha hali ya amani na utulivu katika kipindi chote cha mbio za mwenge wa uhuru ulipokuwa Mkoani Katavi.
Mwenge wa uhuru ulianza mbio zake Mkoani Katavi Julai 10 hadi 14 ukitokea Mkoani Rukwa na Julai 15 kupokelewa katika Wilaya ya Uvinza Mkoani Kigoma.
Kauli mbiyu mwaka huu inasema ‘’Vijana ni nguvu kazi ya taifa,washirikishwe na wawezeshwe’’

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA