MIRADI 9 YAZINDULIWA NA MWENGE WA UHURU MANISPAA YA MPANDA

ZAIDI ya miradi 9 ikiwemo Stendi Mpya ya kisasa ya mabasi katika Manispaa ya Mpanda mkoani Katavi imezinduliwa leo.
Vijana wakimbiza mwenge wa uhuru(PICHA NA Issack Gerald)
                                      

Miradi hiyo imezinduliwa na kiongozi wa mbio za mwenge mwaka huu Bw.George Jakson ambapo amesema miradi hiyo itasaidia kukuza maendeleo ya jamii pamoja na uchumi wa mkoa.
Baadhi ya wananchi walioshiliki katika uzinduzi wa miradi hiyo wamesema wanashukuru kwa kuzinduliwa kwa miradi hiyo ambapo wameiomba serikali kuwasaidia vifaa vya kisasa  ili kuboresha maendeleo yao kutokana na shughuli za kiuchumi wanazozifanya kila siku.
Hata hivyo mwenge wa uhuru leo unakesha katika viwanja vya shule ya msingi Kashato Manispaa ya Mpanda ambapo kesho unatarajia kuelekea katika halimashauli ya mpya ya Tanganyika mkoani Katavi na hatimaye utakabidhiwa Wilaya ya Uvinza Mkoani Kigoma.
Mwandishi:Issack Gerald Bathromeo
Mhariri: Issack Gerald Bathromeo
Habarika zaidi na P5TANZANIA.BLOGSPOT.COM


Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA