AHUKUMIWA JERA MIEZI 6 AU FAINI KWA SHAMBULIO LA KUTUMIA MWIKO



MAHAKAMA ya mwanzo mjini Mpanda imemuhukumu mtu mmoja mkazi wa Shanwe  kifungo  cha miezi 6 jera au kulipa faini  ya  shilingi laki mbili.

Akisoma hukumu hakimu mkazi wa mahakama hiyo mh, sylivesta Makombe  amemtaja mshitakiwa  kuwa ni Shabani Halfan (28) Mkazi wa shanwe tarafa ya Misunkumilo ambapo alimshambulia   Cosmas Galimoshi  kwa kumpiga na mwiko sehemu za kichwani na kumsababishia maumivu makali.
Kwa upande wake mshitakiwa  alipopewa nafasi ya kujitetea amekiri kutenda kosa hilo na ameiomba mahakama impunguzie adhabu kwa kitendo alichokifanya  kwani alifanya bila kukusudia na alikuwa ametumia kilevi.
Mahakama imemhukumu mshitakiwa huyo na kumtaka amlipe bw,Galimoshi  fidia za matibabu  kiasi cha shilingi elfu hamsini ,na adhabu hiyo imetolewa  ili iwe fundisho kwa wengine wenye tabia kama hii.
Mwandishi: Issack Gerald Bathromeo
Mhariri:Issack Gerald Bathromeo
Endelea kuhabarika na P5TANZANIA.BLOGSPOT.COM

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA