WANAKIJIJI KASOKOLA MKOANI KATAVI WAKATAA TAARIFA YA MAPATO NA MATUMIZI,KUSOMWA UPYA MEI 12 MWAKA HUU.


Wananchi wa kijiji cha kasokola kata ya kasokola manispaa ya mpanda wameikataa taarifa ya mapato na matumizi iliyosomwa  katika mkutano wa hadhara ambapo haijasomwa takribani mwaka mmoja na miezi mine.

Wananchi hao wamesema kuwa taarifa hiyo ina mapungufu mengi ikiwemo baadhi ya michango kutoingizwa katika taarifa hiyo hali ambayo imepelekeaa sintofahamu baina ya wananchi na viongozi waliohusika katika kuandaa taarifa hiyo.
Hali hiyo imepelekea mkutano huo kuahirishwa hadi may 12 kutokana na baadhi ya wajumbe wa serikali ya kijiji hicho ambao ndiyo waliohusika kuandaa taarifa hiyo kutohudhuria mkutano huo.
 Kwa upande wake mwenyekiti wa kijiji hicho cha kasokola Bw. Dominic Fungameza amesema yeye hahusiki na tuhuma hizo za ubadhilifu wa fedha za wananchi.

Mwandishi: Judica Schone
Mhariri ;Issack Gerald
Endelea kuhabarika na P5TANZANIA.BLOGSPOT.COM

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA