WAWILI WAKAMATWA WAKITUHUMIWA KUIBA MTOTO WILAYANI MPANDA


Na.Vumilia Abel
SERIKALI  ya kijiji cha Ikaka kata ya Mnyagala Wilayani Mpanda mkoani katavi kimewakamata watu wawili wanaofahamika kwa majina ya Edefance John na Januari Kisulo wote wakazi wa kijiji cha  Isengule kata ya Ikola  kwa tuhuma za wizi wa mtoto mwenyeumri wa miaka 13.

Taarifa ya kukamatwa kwa wezi hao imebainishwa juzi na Afisa mtendaji wa kijiji hicho Bw. Bw.leonard Michael Mbogambi kupitia kikao cha hadhara kilichwashirikisha wananchi kikilenga kujadili kusoma mapato na matumizi ya mradi wa maji.
Aidha mtendaji huyo amesema,watu hao waliokamatwa watapelekwa katika vyombo vya sheria na kuwa ili iwe fundisho kwa watu wenye tabia kama hiyo.
Awali mwenyekiti wa kijiji hicho B w.Mipawa Pikipiki alisema kuwa watu hao aliwapokea majira ya saa 4 asubuhi wakiomba hifadhi ya kulala nyumbani kwake ili kesho yake waendelee na safari ambapo hakufahamu kuwa mtoto waliyekuwa naye siyo wao.
Kwa upande wake askari wa sungusungu wa kijiji hicho Bw.Fredy Nkana Tung’ombe ametoa lawama kwa wazazi juu ya tukio kwa kutomtimiza mahitaji muhimu ya mtoto.
Kwa kwa mujibu wa askari huyo, mtoto huyo ambaye hata hawezi kujieleza amekosa mahitaji ya msingi ikiwemo elimu,mavazi na chakula.
Kwa upande wa watuhumiwa,wamekana kuiba mtoto ambapo wamedai kuwa walifuatwa na mtoto huyo baada ya kumwomba awaoneshe njia ya sehemu wanakoelekea.
Kwa upande mama mzazi wa mtoto huyo Bi.Pascharia Valentino ambaye ni mkazi wa kijiji cha Kalofesi amesema alikuwa akiishi na watu hao kwa mwezi mmoja mpaka sasa.

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA