RPC KATAVI ATAKA SILAHA ZISALIMISHWE


Na.Issack Gerald-Katavi
Jeshi la Polisi Mkoa wa Katavi limewataka wananchi wanaomiliki silaha kinyume cha sheria kuzisalimisha mara moja silaha hizo katika vituo vya Polisi vilivyopo karibu na makazi yao.

Agizo hilo limetolewa na Kaimu kamanda wa Polisi Mkoani Katavi ACP Rashid Mohamed Kwani halitositakisema kuwa hatua kali za kisheria zitachukuliwa kwa mtu au kikundi kitakachobainika kumiliki silaha kinyume cha sheria na taratibu za nchi.
Aidha, Kamanda walio na silaha majumbani mwao ambazo zilikuwa zikimilikiwa kihalali na kwa sasa ndugu zao aliyekuwa akimiliki silaha hiyo alikwishariki dunia wafuate utaratibu kwa kuzisalimisha silaha hizo ambapo suala hili linawahusu pia wazee ambao wamefikisha umri ambao hauwaruhusu kumiliki silaha.
Hata hivyo amesema kuwa ni kosa kisheria wanaomiliki silaha kisheria kuziazimishwa kwa makampuni bina binafi ya ulinzi ambapo pia amewataka kuacha tabia hiyo mara moja.
Kamanda Mohamed amesema kuwa wananchi wanatakiwa kuendelea kutoa ushirikiano kwa jeshi la polisi wanapoona viashiria vyovyote vya uharifu ili vidhibitiwe kabla ya kuleta madhara.

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA