JESHI LA ZIMAMOTO WALALAMIKIWA NA WAKAZI KATAVI KWA KUWAPA VITISHO WENYE MFUMO WA UTAPELI


NA.Issack Gerald-Katavi
Wafanyabiasha wa soko la Buzogwe wamelalamikia hatua ya kikosi cha zima moto Manispaa ya Mpanda mkoani wa Katavi  kwa kuwatoza kodi ambayo haijulikani inakopelekwa pamoja na kutoelimishwa juu ya michango hiyo.
Mwonekano wa gari la zimamoto (PICHA NA Issack Gerald)
                              

Wakizungumza katika mkutano ulioitishwa na uongozi wa soko hilo,wamesema kikosi hicho  kinawatoza kodi ya Shilingi Elfu Arobaini.
Wamesema kuwa askari hao wamekuwa wakiwapa vitisho vya kuwapeleka mahakamani na kuonesha ubaguzi kwa baadhi ya wafanyabiahara kuhusu kulipa kodi hiyo huku wengine wakiwa hawalipi kabisa.
Kwa upande wake mwenyekiti wa soko hilo Bw. Ramadhani Karata amekiri askari hao kuwatisha wafanyabiashara na kuwakuzia faini kwa wale ambao hawajalipa licha ya kuwa hawana elimu kuhusu michango hiyo.
Akijibu malalamiko hayo, Mkaguzi Mkuu wa jeshi la zimamoto na uokoaji Mkoa wa katavi Kamanda Edward Kakwale amesema, kodi hiyo ni ya serikali nzima inayojulikana kama kodi ya ukaguzi zimamoto ambayo hutozwa kwa wafanyabiasha walio na maduka yanayotambulika kisheria.
Aidha Kamanda Kakwale amesema kodi hiyo hulipwa  mara moja kwa mwaka mzima na hupelekwa katika mfuko wa serikali kwa ajili ya majukumu mengine ya kiserikali.

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA