MWANASHERIA MKUU WA SERIKALI MKOA WA KATAVI AFIKISHWA MAHAKAMANI AKITUHUMIWA KUMTOROSHA ALIYETAKA KUMUUA KWA KUKATA KIGANJA CHA MKONO MLEMAVU WA NGOZI ALBINO,WAMO PIA ASKARI MAGEREZA WAWILI WILAYANI MPANDA NA WALIOKUWA WAKITOROSHWA WADAKWA TENA.


Na.Issack Gerald-Katavi
Watu watano akiwemo Mwanasheria Mkuu Mkoani Katavi Bw. Falhati Seif  Khatibu (45),wamefikishwa katika mahakama ya Wilaya ya Mpanda kwa tuhuma za kumtorosha mtuhumiwa  Alex Manyanza Enock (27) Mkazi wa majimoto aliyekuwa anakabiliwa na kesi NA. MTO/IR/76/2015 ya kujaribu kuua mlemavu wa Ngozi Albino Limi Luchoma(30) mkazi wa kijiji cha Mawiti kata ya Majimoto Wilayani Mlele.
                                      

Kaimu kamanda wa Polisi Mkoani Katavi Rashid Mohamed,amewataja watuhumiwa kwa ujumla kuwa ni A. 287 Sajenti John Musa (50) mkazi wa mtaa wa mji mwema Wilayani Mpanda, A. 5385 Sajenti Deogartius Katani (50) Mkazi wa mtaa wa Kigamboni Wilaya ya Mpanda wa gereza la mahabusu Mpanda.
Kamanda pia amewataja wengine wanaotuhumiwa kuwa ni Mwanasheria mkuu wa Mkoa wa Katavi   Falhati Seif  Khatibu (45) mkazi wa maeneo ya Msakila Shule ya Msingi ,Masanja Kasinje Kasala(33) mkazi wa Kakese Mkwajuni Wilayani Mpanda pamoja na Ngassa Mashindike (37) mkazi wa Majimoto Wiayani Mlele.
Kamanda Mohamed amesema kuwa mnamo 19.01.2016 majira ya saa 09:30 asubuhi,Jeshi la Polisi Mkoani Katavi lilipokea taarifa toka kwa raia wema kuwa mtuhumiwa  Alex Manyanza Enock hayupo gereza la mahabusu Mpanda.
Baada ya taarifa hizo kupokelewa,jeshi la polisi lilianza upelelezi na kubaini kuwa mtuhumiwa huyo alitoroka tangu tarehe 12.10.2015 katika gereza la mahabusu Mpanda ambapo awali mtuhumiwa huyo aliwahi kutoroka akitumikia kifungo cha miaka 5 kwa kosa la wizi wa mifugo katika gereza la kilimo la Kalilankulukulu kabla ya kukamatwa kwa kesi hii ya kujaribu kuua.
Kamanda ameendelea kufafanua kuwa,ilipofika 21.01.2016 wakati jeshi la polisi likiendelea na upelelezi wa kesi hiyo,zilipokelewa taarifa za kuwa mtuhumiwa Alex Manyanza Enock anapatikana Mkoani Rukwa ambapobaada ya ufuatiliaji,mtuhumiwa alipatikana akiwa amejificha katika kijiji cha Kipande Wilayani Nkasi Mkoani Rukwa.
Katika mahojiano ya kina,mtuhumiwa Bw. Alex Manyanza Enock alieleza jinsi alivyofanikishiwa mipango ya kutoroka gerezani akimtaja mjomba wake Bw.Masanja Kasinje Kasala pamoja na rafiki yake Ngassa Mashindike ambao naobaada ya kukamatwa walikiri kufanya mipango ya kumtorosha mtuhumiwa kwa lengo la kuwafanya watuhumiwa wengine katika kesi yao ya kujaribu kuua kutotiwa hatianki akiwemo mjomba wake walioko pamoja katika kesi hiyo Bw.Masunga Kashinje.
Mtuhumiwa alieleza kuwa waliwashirikisha askari magereza wawili ambao ni A. 287 Sajenti John Musa Masagula na  A. 5385 Sajenti Deogratius Katani wote wakazi wa kituo cha kazi gereza la mahabusu Mpanda ambao walipatiwa  kiasi cha Shilingi  milioni moja(1,000,000/= ) ili kumwezesha mtuhumiwa kutoroka.
Pia walimtaja mwanasheria mkuu wa serikali ya Mkoa wa Katavi Bw. Falhati Seif  Khatibu  ambapo walidai walimpatia kiasi cha shilingi milioni mbili (2,000,000/=)ili kumwondolea shitaka mtumiwa Masunga Kashinje baada ya kuwa mtuhumiwa Alex Manyanza Enock amefanikiwa kutoroka.
Hata hivyo,Kamanda wa polisi Mkoani Katavi ametoa wito kwa watumishi wa umma na wale wa sekta binafsi kufanya kazi kwa kufuata misingi ya utumishi huku wakiendelea kuihudumia jamii kwa ukaribu.
Mshirikishe na mwenzako

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA