MKURUGENZI HALMASHAURI YA WILAYA YA NSIMBO ATAKA WANAFUNZI WASOME MASOMO YA SAYANSI


Na.Agness Mnubi-Nsimbo.
WANAFUNZI wa Shule za Sekondari katika Halmshauri ya Wilaya ya Nsimbo Mkoani katavi wametakiwa kusoma masomo ya sayansi.

Wito huo umetolewa leo na Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo Bw. Michael Nzyungu wakati akizungumza na P5 TANZANIA MEDIA sambamba na Mpanda redio,akisema kuwa wanafunzi wajitokeze kwa wingi kusoma masomo ya sayansi ili kufaidi maabara zilizopo katika shule za sekondari za Halmashauri ya Nsimbo.
Amesema Lengo la Serikali kujenga maabara kila shule ya sekondari ni kuinua kiwango cha elimu kwa masomo ya sayansi hivyo wanafunzi hawana budi kusoma masomo ya sayansi ili kutumia maabara hizo.
Amesema wanazidi kuboresha maabara hizo kwa kuhakikisha kuwa na  miundombinu mizuri, kuongeza  vifaa vya kutosha na walimu wa masomo ya sayansi.
Kauli ya mkurugenzi mtendaji huyo inakuja ikiwa ni njia mojawapo ya kuhamasisha wanafunzi kusoma masomo ya sayansi kwa lengo la kupata wataalamu katika masuala mbalimbali hapa nchini.
Hata hivyo licha ya hamasa hiyo,kunahitajika walimu zaidi wa masomo ya sayansi wenye uwezo thabiti.



Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA