KESI YA KUVUNJA DUKA YAENDELEA KULINDIMA MPANDA,HAKIMU ATUPILIA MBALI OMBI LA MSHTAKIWA


Na.Issack Gerald-Mpanda
KESI ya kuvunja duka na kuiba nguo zenye thamani ya shilingi milioni moja na laki nne na elfu arobaini, inayomkabili Bw. Reuben Remmy mkazi wa Makanyagio,mwishoni mwa wiki ya Januari,imeendelea kusikilizwa katika mahakama ya Mwanzo mjini Mpanda.

Ushahidi uliotolewa mbele ya Hakimu wa mahakama hiyo Bw. David Mbembela ni pamoja na vielelezo vya makufuli mawili yaliyovunjwa siku ya tukio usiku wa tarehe 28 mwezi desemba mwaka jana mjini Mpanda.
Shahidi wa sita askari wa jeshi la polisi Mpanda kitengo cha upelelezi, Selcius Mosha, ameithibitishia mahakama kuwa vielelezo hivyo ni sahihi na vimetambuliwa na mlalamikaji Bi. Rosana Mwancheta pamoja na mashahidi wengine. 
Hakimu Mbembela amesema mahakama imetupilia mbali pingamizi lililotolewa na mshtakiwa la kuiomba isitambue vielelezo hivyo, na kwamba mshtakiwa ana kesi ya kujibu.
Kesi hiyo imeahirishwa hadi tarehe 15 mwezi Februari mwaka huu itakaposikilizwa tena.

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA