WANAFUNZI 1137 WATOKOMEA KUSIKOJULIKANA,AFISA ELIMU KUTANGAZA MSAKO NYUMBA KWA NYUMBA.


Na.Issack Gerald-Nkasi.
WANAFUNZI wapatao 1137 kati ya 2257  hawajaripoti shule kuanza kidato cha kwanza mwaka huu katika Wilaya ya Nkasi Mkoani Rukwa licha ya serikali kutoa elimu bure.

Akizungumza na P5 TANZANIA MEDIA sambamba na  Mpanda Radio kwa njia ya mawasiliano ya simu Kaimu Afisa Elimu sekondari  Wilayani Nkasi Bw. Fortunatus Kaguo amesema kuwa,jumla ya wanafunzi 2257 walichaguliwa kuanza  kidato cha kwanza mwaka huu lakini hadi sasa walioripoti shuleni ni wanafunzi 1120 pekee huku wengine1137 wakiwa hawajulikani walipo.
Aidha Afisa elimu huyo amewataka wazazi  kuwapeleka watoto wao shule na atakayekaidi atachukuliwa hatua kali  za sheria.
Amefafanua kuwa wanamikakati ya kuanzisha oparesheni ya nyumba kwa nyumba ili kuwasaka wazazi ambao hawajawapeleka watoto wao shule.
 Hatua ya kukosekana kwa wanafunzi hawa kunafuatia ikiwa ni  muda mfupi baada ya Seriklai kutangaza mpango mkakati wa elimu bure kwa wanafunzi kuanzia Chekechea hadi sekondari kwa wanafunzi wa kidato cha nne.

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA