JESHI LA POLISI KATAVI LASHAURIWA KUZUIA UHARIFU BADALA YA MATUKIO


Na.Issack Gerald-Katavi
Jeshi la polisi mkoani Katavi limeshauriwa kujenga desturi ya kuzuia uharifu kabla haujatokea badala ya kupambana na matukio
Agizo hilo limetolewa na mkuu wa mkoa wa Katavi, Dr. Ibrahim Msengi wakati wa maadhimisho ya siku ya Polisi nchini iliyofanyika Juzi katika viwanja vya Polisi Wilayani Mpanda.
Dr. Msengi amesisitiza kuwa endapo jeshi la polisi litawatumia askari wake kufanya tafiti na kushirikisha wananchi katika ukusanyaji wa taarifa, uharifu utadhibitiwa kabla haujaleta madhara.
Kwa upande wake mkuu wa jeshi la polisi mkoa wa Katavi ACP Dhahiri Kidavashari amekiri kuwepo kwa mafanikio pamoja na changamoto ambazo zitafanyiwa kazi ili kuimarisha usalama.
Kwa upande wake Kamanda wa Polisi Mkoani Katavi Dhihiri Kidavashari aliwapongeza wananchi wanaoendelea kuonesha ushirikiano wa kuwabaini waharifu wa vitendo mbalimbali

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA