ASHIKILIWA NA POLISI KATAVI KWA KUKAMATWA NA METO YA TEMBO KILOGRAM 50 YENYE THAMANI YA SHILINGI MIL.120.


Na.Issack Gerald-Katavi
Mtu mmoja aliyefahamika kwa jina la Nzuri Ndizu (44) mkazi wa kijiji cha mbede anashikiliwa  na Jeshi la Polisi akiwa na meno 08 ya tembo vyenye uzito wa kg 50 ikiwa na thamani ya Tshs 120,000,000/= ambapo ni sawa na tembo 4 waliouawa kinume cha sheria.
Mtuhumiwa bw.Nzuri Ndizu akiwa Polisi kwa Mahojiano baada ya kukamatwa na meno ya tembo(PICHA na.Issack Gerald)
                                                                 
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Katavi akifafanua kuhusu kukamatwa kwa mtuhumiwa wa meno ya tembo
                                                                                    
Meno ya tembo yaliyokamatwa haktika hatua ya kusubiri kuuzwa


Akithibitisha kukamatwa kwa mtuhumiwa huyo,Kamanda wa polisi Mkoani Katavi Dhahiri Kidavashari amesema kuwa mtuhumiwa huyo ametenda kosa hilo mnamo tarehe 08.01.2016 majira ya saa 3 na nusu usiku kwenye pori la akiba la Lwafe Wilayani Mlele Mkoani Katavi.
Kamanda Kidavashari amesema kuwa,Jeshi la Polisi lilipata taarifa toka kwa raia wema kuwa katika pori la akiba la Lwafe kuwa kuna watu wanajihusisha na biashara haramu ya meno ya tembo na kuanza kufuatilia taarifa hizo na hatimaye kumkamata mtuhumiwa Nzuri Ndizu  akiwa na vielelezo hivyo vilivyokuwa vimefichwa porini kusubili wateja.
Hata hivyo jeshi la polisi linaendela na uchunguzi zaidi
kubaini mitandao yote inayojihusisha na biashara hivyo haramu ya meno ya tembo ambapo mtuhumiwa atafikishwa afikishwa mahakamani baada ya upelelezi kukamilika.

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA