JAMII MWANZA YATAKIWA KUTAWANYANYAPAA WAATHIRIKA WA DAWA ZA KULEVYA


Na.Issack Gerald-Mwanza.
Jamii nchini imetakiwa kutowanyanyapaa waathirika wa dawa kulevya badala yake iwasaidie kuondokana na matumizi ya dawa hizo ikiwemo kuwafikisha katika vituo vya utimamu wa akili (Sobar House).

Rai hiyo imetolewa Bw Eddy Darkis Meneja wa Kituo cha Utimamu wa akili cha Back To Life Sobar House  Pasiansi Manispaa ya Ilemela Mkoani Mwanza, ambacho husaidia wahanga wa dawa za kulevya kuachana na matumizi ya dawa hizo.
Bw Darkis amesema kuwa badhi ya wanajamii wamekuwa wakiwanyanyapaa wahanga wa dawa za kulevya, jambo ambalo linakwamisha mapambano dhidi ya matumizi ya dawa hizo nchini ambapo  wahanga zaidi ya 50  wamepatiwa tiba huku wengine 25 wakiendelea vizuri.
Ripoti ya Mwenyekiti wa chama cha waandishi wa wa habari za kupiga vita uharifu, biashara na matumizi ya dawa za kulevya nchini OJADACT Bw Edwini Soko Miezi 6 ili yopita,idadi ya watumiaji wa dawa za kulevya Jijini Mwanza imefikia zaidi ya watu elfu kumi.
Asante kwa kuendelea kuchagua P5 TANZANIA MEDIA
Chanzo:Mwandishi wetu Mwanza

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA