AFIKISHWA MAHAKAMANI KWA SHAMBULIO LA MME WAKE




Na.Issack Gerald-Mpanda
MTU mmoja mkazi wa Kawajense katika Manispaa ya Mpanda, Bi. Judith Mgawe, juzi amefikishwa katika mahakama ya Mwanzo mjini Mpanda akikabiliwa na shtaka la shambulio la kudhuru mwili dhidi ya mmewe.

Akisoma shtaka hilo mbele ya hakimu wa mahakama hiyo Bw. David Mbembela, Koplo Mtei wa jeshi la polisi Mpanda amesema mshtakiwa alitenda kosa hilo January 8 mwaka, kwa kumpiga mmewe Bw. Kasanga Mgamba kwa kutumia kipande cha ubao na kumsababishia maumivu makali..
Hakimu Mbembela ameruhusu dhamana kwa mshtakiwa, lakini mshtakiwa alikosa mdhamini na kulazimika kudhaminiwa na Bibi yake, baada ya mahakama hiyo kulinda maslahi ya mtoto mdogo aliye naye. 
Mshtakiwa amekana shtaka hilo na kesi hiyo imeahirishwa hadi tarehe 3 mwezi Februari mwaka huu itakaposikilizwa tena.

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA