WANAFUNZI KIDATO CHA SITA WAANZA MTIHANI WA MOCK KIKANDA


Na.Issack Gerald-MPANDA
WANAFUNZI wa kidato cha sita katika Manispaa ya Mpanda wameanza kufanya mtihani wa mock.

Akizungumza na P5 TANZANIA MEDIA,Afisa elimu idara ya elimu ya sekondari Bi.Lutungulu Eliya amesema pamoja na kufanya mtihani wa mock,wamejiandaa kufanya vizuri katika mtihani wa Taifa utakaofanyika mwezi Machi mwaka ujao.
Hata hivyo Bi.Eneliya amezitaja chanamoto zinazowakabiri kuwa ni pamoja na ukosefu wa walimu wa masomo ya hesabu kutokana na wanafunzi kuongezeka na kufikia 759 ambapo kati yao walio wengi wanasoma masomo ya sayansi.
Wakati huo huo  serikali imeombwa kuongeza vifaa vya kutosha vya sayansi ili kupata wataalam watakaokuwa msaada kwa jamii.    

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA