WAFANYABIASHARA,WANUNUZI WAILALAMIKIA SERIKALI KUPANDISHA BEI YA BIDHAA


Na.Issack Gerald-MPANDA
BAADHI ya Wanunuzi na wafanyabiashara wadogo wadogo wilayani Mpanda mkoani Katavi wameilalamikia serikali kutokana na kupandisha bei za bidhaa nchini kiasi kinachowafanya washindwe kuyamudu maisha yao.

Malalamiko hayo yametolewa leo na wafanyabiashara wanunuzi wakati wakizungumza na mpanda redio, kutokana na kuongezeka kwa viwango vya bei kwenye bidhaa hasa  vyakula, na kudai kuwa itawafanya kuendelea kuwa maskini kutokana na kipato chao kuwa cha chini.
Aidha wameiomba serikali mpya iliyoingia madarakani kuangalia kipato cha mwananchi mmoja mmoja na kupanga bei zinazolingana na kipato halisi cha Mtanzania.
Kwa mujibu wa takwimu zilizotolewa na Mkurugenzi wa sensa ya watu na takwimu za jamii Bw. Ephraim Kwesigabo  zinaonyesha kuwa mfumko wa  bei za bidhaa umeongezeka hadi asilimia 6.3 kutoka asilimia 6.1 mwezi septemba mwaka huu.

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA