MIL.80 ZATUMIKA KUSAIDIA KAYA 62 ZILIZOATHIRIWA NA MVUA,WAFANYABIASHARA NAO KUFANYIWA TATHMINI


Na.Issack Gerald-SUMBAWANGA
Zaidi ya Shilingi Milioni 80 zimetumika kuwasaidia wahanga wa mvua iliyombatana na upepo Mkali Oktoba mosi mwaka huu.

Akizungumza na P5 TANZANIA MEDIA Kwa njia ya Simu ,Mratibu wa maafa Mkoani Rukwa Bi.Aziza Ramadhani amesema ,tahmini ambayo imefanyika, imeonesha Jumla ya Kayazipatazo  62 zimebainika kuathiliwa vibaya sana na mvua hiyo.
Aidha amesema,tathmini inaendelea kufanyika ili kuwalipa fidia wafanyabiashara ambao  biashara zao zimeharibiwa na mvua hiyo ikiwemo magunia zaidi ya 300 ya vyakula mbalimbali katika maeneo ya sokoni.
Mbali na Mamlaka ya hali ya hewa Tanzania kutoa tahadhari ya mvua za Elinino za mwaka huu kila mara ,Bi.Aziza amewashauri wakazi wa Mkoa wa Rukwa kupanda miti inayozunguka kuzuia upepo pamoja na kutoziba mifereji inayopitisha maji kuepusha maji kupenya katika makazi ya watu.

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA