ASKARI WA WANYAMAPORI KATAVI WALALAMIKIWA KWA UDHALILISHAJI WA RAIA NSIMBO


Na.Masoud Mmanywa-Nsimbo
WAKAZI wa kijiji cha Mtisi Kata ya Stalike wilayani Nsimbo mkoani Katavi, wamewalalamikia askari wa Wanyamapori kwa kuwapiga na kuwajeruhi kwa madai ya kuwakuta wakilima katika eneo la hifadhi ya msitu.

Wakizungumza katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika kijiji cha Mtisi, wamesema wamekuwa wakisumbuliwa na askari wa wanyamapori kwa kuwapiga hadi kuwajeruhi na kusababisha shughuli za kilimo ambazo ndiyo tegemeo la wakazi hao kutofanyika na kuishi kwa wasiwasi.
Miongoni mwa watu waliopigwa ni Bw. Salamo Kayange mkazi wa kijiji cha Mtisi.
Mwenyekiti wa kijiji cha Mtisi Bw. Pius Tito Mwantepela amesema kuwa, baada ya matukio hayo ya kupigwa kwa wakazi wa kijiji hicho serikali ya kijiji imeshawasiliana na ofisi ya maliasili na wamekiri kufanya oparesheni katika maeneo ya hifadhi.
Amesema kuwa tatizo hilo ni la muda mrefu na hadi sasa halijapatiwa ufumbuzi na kwamba kijiji hicho kilishaandika maombi ya kupewa ardhi itakayotumika kwa kilimo, kwani kijiji hicho kilichoanzishwa mwaka 1982, kina ufinyu wa ardhi kutokana na kupakana na migodi pamoja na eneo la hifadhi.

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA