BAADHI YA VIFAA VYA KUPIGIA KURA VYAWASILI MANISPAA YA MPANDA


Na.Issack Gerald-MPANDA.
Manisapaa yaMpanda Mkoani katavi imepokea baadhi ya vifaa ambavyo vitatumika katika upigaji kura Oktoba 25 mwaka huu.

Hayo yameelezwa na Afisa Uchaguzi Manispaa ya Mpanda Bw. Reginald Clavery wakati akizungumza na Mpanda Radio Ofisini kwake.
Amevitaja miongozni mwa vifaa ambavyo vimewasilishwa kuwa ni pamoja na karatasi za kujaza matokeo ya kura,kalamu,taa na vituturi ama meza za kuandikia
Aidha amesema kuwa wamepokea karatasi za maandishi nundu kwa ajili ya watu wenye ulemavu wa kutoona ili kuwawezesha kupiga kura wenyewe kuliko kutumia mtu mwingine kuwakilisha kura yake.

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA