TWAWEZA WATANGAZA MATOTKEO YA UTAFITI CCM YAONGOZA,WAKAZI KATAVI WAONYA


 
Baadhi ya wakazi katika Picha wakijadili matokeo yaliyotangazwa na Taasisi ya twaweza jana Jijini Dar es Salaam

Issack Gerald-Katavi
Baadhi ya wakazi Mkoani Katavi wameitaka tume ya uchaguzi na tume ya haki za binadamu kufanya uchunguzi na kutorusu utafiti wa kutangaza matokeo kabla ya uchaguzi kufanyika.

Wakizungumza na P5 TANZANIA wakazi hao wamesema kutoa matokeo ya utafiti kabla ya uchaguzi kunaweza kuligawa taifa na kupelekea uvunjifu wa amani nchini.
Kauli ya wakazi hao inakuja ikiwa ni saa chache baada ya Taasisi isiyo ya kiserikali ya Twaweza kutangaza matokeo ya utafiti wake.
Utafiti huo umeonesha kuwa endapo uchaguzi ungefanyika mwezi mmoja uliopita, mgombea urais wa CCM John Magufuli angepata ushindi kwa asilimia 65.
Matokeo ya utafiti huo ambao  umetolewa leo jijini Dar es salaam unaonesha pia kuwa wagombea wa CCM katika ngazi zote ikiwa ni pamoja na ubunge na udiwani CCM inaongoza.

Katika ngazi ya udiwani CCM imeongoza kwa asilimia 60 ikifuatiwa na CHADEMA asilimia 24 na ngazi ya ubunge CCM imeongoza kwa asilimia 60 ikifuatiwa na CHADEMA yenye asilimia 26, wakatika katika ngazi ya urais bila kujali mgombea, CCM imeongoza kwa asilimia 66 ikifuatiwa na CHADEMA asilimia 22 huku chama cha ACT Wazalendo kikifuatia kwa kuungwa mkono na wananchi kwa zaidi ya asilimia 1%.
Siku chache zilizopita Asasi za kiraia AZAKI ikiwemo TWAWEZA,  zilizindua ilani ya uchaguzi mkuu wa mwaka 2015 na kuzuia kauli zenye mwelekeo wa uchochezi na utabiri wa matokeo ya uchaguzi wa mwaka huu.


Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA