RPC KATAVI KUHITISHA KIKAO CHA KUJADILI AMANI KESHO KIKISHIRIKISHA WAZEE MAARUFU


Na.Issack Gerald-KATAVI
JESHI la polisi Mkoani Katavi kesho linatarajia kuwa na kikao maalumu cha kujadili mikakati ya kuimarisha amani na usalama wa nchi.

Kikao hicho ambacho kinaandaliwa na Kamanda wa jeshi la polisi Mkoani Katavi kikishirikisha wazee maarufu,wanasiasa na viongozi wa dini kinalenga kujadili namna ya kuakikisha usalama unakuwepo kipindi cha kampeni kuelekea uchaguzi mkuu Oktoba mwaka huu.
Miongoni mwa ambayo yamekuwa yakitajwa kuhatarisha amani ya nchi ni pamoja na Lugha za uchochezi kutoka kwa wanasiasa na wafuasi wao na kutozingatia taratibu na miongozo ya uendeshaji kampeni.
Kikao hicho ni cha pili baada ya kile kilichofanyika Septemba 11 ambapo pia wanatarajia kujadili ikiwa yale yaliyojadiliwa katika kikao kilichopita yametekelezwa.

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA