WAKULIMA,WAFUGAJI MPANDA WATOA MAONI KUHUSU SHEREHE ZA NANENANE


NA.Issack Gerald-Mpanda
SIKU mbili baada ya maonesho ya kilimo na ufugaji  maarufu kama nane nane, baadhi ya wakulima  pamoja na wafugaji Mkoani Katavi wametoa maoni na mapendekezo kuhusu sekta ya kilimo.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti mapema jana wakulima hao walisema kuna umuhimu mkubwa kwa serikali kuanza kutatua changamoto zinazowakabili wakulima.
Changamoto mbali mbali zimetajwa kuwa kikwazo kwa wakulima nchini katika kufikia adhma ya kuzalisha mazao kwa kiwango bora.
Wametaja changamoto hizo kuwa ni pamoja na Uhaba wa masoko, kukosekana kwa pembejeo za kilimo pamoja na migogoro ya ardhi.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk.  Jakaya Kikwete akiwa mgeni rasmi katika kufunga  maonesho ya nane nane kitaifa yaliyofanyika mkoani Lindi amesema serikali itaelekeza nguvu zaidi katika kukabiliana na changamoto za kilimo.



Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA