WATOTO WA KANISA KATOLIKI WATOA MSAADA KWA WAGONJWA HOSPITALI YA MANISPAA YA MPANDA


Katika kuadhimisha Alhamisi kuu kuelekea sikukuu ya pasaka,Watoto wa shirika la mtoto yesu kutoka jumuiya mtakatifu Filomena kigango cha Kawajense Majengo Mapya jimbo katoliki la Mpanda Mkoani Katavi,wametoa msaada wa vitu mbalimbali kwa wagonjwa waliopo katika Hospitali ya Manispaa ya Mpanda.

Wakizungumza kwa niaba ya watoto wenzao Sesilia John Enock na Samweli wamesema wameamua kutoa msaada kwa wagonjwa wenye uhitaji ikiwa ni kuadhimisha Alhamisi kuu katika kuelekea sikukuu ya pasaka.
Jimbo Katoliki la Mpanda Katavi(PICHA NA.Issack Gerald)
Kwa upande wake Katekista Joseph Paul Kansato ambaye pia ni mwalimu wa parokia ya kanisa kuu jimbo la Mpanda amesema watoto hao wametoa misaada mbalimbali ikiwemo sabuni, mafuta na sukari kama ishara ya upendo walionao kwa watu wenye shida mbalimbali.
Kwa upande wao baadhi ya wagonjwa wakiwemo Mussa Paul na Magreth Peter Ndekeja wametoa shukrani zao kwa watoto hao waliotoa msaada huo huku wakiomba jamii kuiga mfano uliooneshwa na watoto hao.
Miongoni mwa wodi ambazo wamezitembelea ni pamoja na wodi ya watoto,akina mama,majeruhi pamoja na wenye uhitaji maalumu.
Maadhimisho ya Alhamisi kuu kuelekea sikukuu ya pasaka Jumapili ya Aprili mosi mwaka huathimishwa na wakristo kote duniani kwa kutekeleza amri ya mapendo kama yesu kristo alivyosema.
Habario zaidi ni WWW.P5TANZANIA.BLOGSPOT.COM  


Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA