MKOANI KATAVI AMUUA MKEWE NA KUZIKA MWILI WAKE


Jeshi  la  Polisi mkoani Katavi  linamshikilia mkazi  wa  Kijiji  cha  Songambele  Kata ya  Sibwesa  Tarafa ya  Karema Wilaya ya  Tanganyika  jina  lake  limehifadhiwa(45) kwa  tuhuma za kumuua mke  wake(31) kwa sababu ya wivu wa kimapenzi na  kisha mzika huku  mtoto wake mwenye  umri wa miaka tisa akishuhudia tukio.
Kamanda wa  Jeshi la  Polisi wa  mkoa  wa  Katavi   Damas   Nyanda    alisema tukio  la kupatikana  kwa  mwili  wa  marehemu  huyo lilitokea juzi majira ya saa 6;00 mchana  katika Kijiji  hicho.
Alisema  marehemu aliuawa  na  mumewe huyo siku ya  januari 15  kwa  kupigwa na  mumewe  kwa  kutumia silaha  zajadi ambazo ni fimbo na  mpini  wa   jembe baada ya  kumtuhumu kuwa  anamahusiano wa  kimapenzi na wanaume  wengine  Kijijini  hapo.
Kamanda   Nyanda alisema wakati mtuhumiwa  huyo akitenda kosa hilo   ambalo  lilishuhudiwa  na  mtoto  wake wa kiume hadi   baba  yake  alivyomuuawa  mama  yake  na  kisha  kuchimba shimo na  kumfukia ardhini.
Baada ya kufanya mauaji  hayo  na kuzika mwili huo mtuhumiwa alirejea  nyumbani  kwake na  kuendendelea  na  shughuli  zake  kama kawaida na  alimtishia  mtoto wake  huyo  mdogo na  kumwambia   asimwambie  mtu  yeyote.
Majirani  waliokuwa  wakimfahamu  marehemu  baada ya  kuona  haonekani  Kijijini  hapo walianza kumuuliza  mtuhumiwa  mahali  alipo  mkewe  naye   alikuwa  akiwajibu kuwa  mkewe  amesafiri kwenda kwao kusalimia.
Kamanda Nyanda alisema Jeshi la  polisi  lilipata  taarifa   ya mauaji ya  mama  huyo  hapo  machi 15 na  ndipo  lilipoanza  uchunguzi wa  tukio  hilo.
Alileza  kuwa baada ya  kufanya  uchunguzi wa kina ndipo juzi   walimtia  mbaroni  mtuhumiwa  na   baada ya  mahojiano  alikiri  kufanya  mauaji  hayo kwa  kile alichodai kuwa  alikasirishwa na  tabia ya  mke  wake ya kuwa na mahusiano ya kimapenzi na wanaume wengine kijijini  hapo  na  aliwaeleza  polisi kuwa  yuko  tayari  kwenda kuwaonyesha alipofukia mwili wa  mke  wake  baada  ya  kufanya mauaji.
Baada ya   mahojiano  hayo  hapo juzi  majira ya saa  6;00 mchana   polisi walifika  kwenye  eneo   ambalo  mtuhumiwa alikuwa  amemfukia  marehemu   mkewe na  baada ya kufukua  eneo  hilo walikuta  mwili na kuutambua kuwa ni mwili wa  mwanamke huyo na kisha kuutoa katika eneo hilo.
Kamanda   Nyanda  alisema mwili   wa  marehemu baada ya kufukuliwa  ulichukuliwa na kupelekwa   katika   chumba  cha  kuhifadhi maiti katika  Manispaa ya  Mpanda.
Mtuhumiwa  anaendelea  kushikiliwa  na  jeshi la  polisi na  mara baada ya  upelelezi kukamilika  anatarajiwa kufikishwa  mahakamani  ili  akajibu  tuhuma zinazo  mkabili.
Habario zaidi ni WWW.P5TANZANIA.BLOGSPOT.COM  

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA