RAIS MAGUFULI AZINDUA KIWANDA CHA SIGARA


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Dkt.John Pombe Magufuli leo amezindua kiwanda cha kutengeneza sigara cha Philips Morris International kilichopo mkoani Morogoro.
Rais Magufuli ametembelea kiwanda hicho na kushuhudia namna sigara zinavyotengenezwa kuanzia katika hatua ya kwanza mpaka sigara inapokamilika kwa matumizi au kwa ajili ya kuuzwa.

Kwa upande wake Mmiliki wa kiwanda hicho amesema kuwa mpaka sasa kiwanda hicho kimeajiri zaidi ya watu mia mbili na ishirini na nne ambao wanahusika katika kuhakikisha uzalishaji unakwenda salama.
Hata hivyo,Rais Dkt.Magufuli amempongeza mmiliki wa kiwanda hicho kwa kuzalisha ajira kwa wingi kwa Watanzania.
Habari zaidi ni P5TANZANIA.BLOGSPOT.COM

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA