WANANCHI WATAKIWA KUTUMIA MAHAKAMA KUPATA HAKI

Wananchi Mkoa wa Katavi wametakiwa kujenga tabia ya kuitumia mahakama kama Chombo cha kupatia haki kama kichocheo cha kuimarisha dhana ya Utawala bora  hapa Nchini.
Katika picha katikati ni Mkuu wa Wilaya ya Tanganyika Salehe Muhando akiwa na Mkuu wa Wilaya ya Mpanda Lilian Charles Matinga
Rai hiyo imetolewa na Mkuu wa wilaya ya Tanganyika Mheshimiwa Salehe Muhando wakati wa uzinduzi wa wiki ya sheria  ambayo imeanza kuadhimishwa katika Viwanja vya mahakama ya wilaya Mpanda.
Kwa upande wake hakimu mkazi mfawidhi wa mahakama mkoani Katavi,MH Ommary Hassani Kingwele amesema dhima kubwa ya uwepo wa wiki ya elimu ya sheria ni kuhakikisha kuwa wananchi wote wanapata uelewa wa sheria.
Madhimisho hayo ya sheria mwaka huu yaliyo na kauli mbiu ‘’matumizi ya tehama katika utoaji haki kwa wakati na kwa kuzingatia maadili’’kilele chake kitakuwa Februari moja mwaka huu na mgeni rasmi anatarajiwa kuwa mkuu wa mkoa wa Katavi meja jenerali mstaafu Rafael Muhuga.

Habari zaidini P5TANZANIA LIMITED

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA