NAIBU WAZIRI AWAKABIDHI SILAHA MADEREVA BODABODA MKOANI KATAVI TAYARI KUPAMBANA NA MIMBA ZA UTOTONI



Na.Issack Gerald
Naibu waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia Wazee na Watoto Dk.Faustine Ndugulile,amewataka waendesha pikipiki Mkoani Katavi kushirikiana na serikali ili kutokomeza mimba za utotoni.
Dk.Ndugulile ametoa agizo hilo leo wakati akitunuku vyeti kwa waendsha pikipiki 100 wa Manispaa ya Mpanda waliohitimu mafunzo ya kidhibiti Mimba za utotoni huku akiwataka pia watendaji wa wizara mpaka wilaya kote nchini kutatua shida zinazowakabili madereva hao.
Wakati huo huo Dk.Ndugulile amekabidhi baiskeli tano kwa wasimamizi wa mashauri ya watoto Manispaa ya Mpanda baiskeli ambazo zimetolewa na shirika la JSI la Marekani ili baiskeli hizo zitumike kuwafikia watoto waishio katika mazingira hatarishi.
Kwa upande wake Mwenyekiti wa waendesha pikpiki Mkoani Katavi Mh.Asalile Mwakabafu amesema wao watahakikisha wanashiriki kudhibiti mimba za utotoni huku akisisitiza serikali kusimamia watendaji wake wasioshughulikia matatizo ya waendesha pikipiki Mkoani Katavi.
Kwa upande wake Chacha Maisol ambaye ni Mkurugenzi wa Shirika la JSI la Marekani upande wa mikoa ya Nyanda za juu Kusini amesema Wizara ya Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa-TAMISEMI iliwaelekeza kutumia nguvu kubwa katika Halmshauri 84 kati ya hizo 83 zikiwa za Tanzania bara na 1 upande wa Zanzibar.
Aidha Maisol amesema katika ukanda wa Nyanda za juu kusini wanatoa huduma katika Halmashauri 23 za mikoa ya Rukwa,Katavi,Songwe,Ruvuma,Njombe na Songwe ambapo jumla ya wasimamizi wa mashauri 500 kutoka katika miko hiyo wamepatiwa mafunzo ili kuelimisha na kudhibiti watoto waishio katika mazingira hatarishi.
Mkoa wa Katavi mpaka sasa unaongoza nafasi ya kwanza kwa asilimia 45 kwa kuwa na watoto wenye mimba za utotoni kati ya mikoa yote Tanzania.
Dk.Ndugulile aliyekuwa ameambatana na watendaji wa wizara yake na wengine kutoka Tamisemi Ofisi ya Rais aliwasili jana Mkoani Katavi na kufanya ziara katika Halmashauri za Mkoa wa Katavi.
Habari zaidi ni P5TANZANIA LIMITED

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA