TAAS MKOANI KATAVI WAMEKATAA KUITWA WALEMAVU WA NGOZI

Na.Issack Gerald
Chama cha watu wenye Ualbino Tanzania (TAAS) Mkoani Katavi kimewataka watanzania kutowaita wao kama watu wenye ulemavu wa ngozi albino badala yake wawaite watu wenye Ualbino.
Mwenyekiti wa TAAS Mkoani Katavi Victus Kweka
Kauli hiyo imetolewa na mwenyekiti wa chama hicho Mkoani Katavi Bw.Victus Kweka kupitia kikao cha kujadili kupinga ukatiri,unyanyasaji na ukandamizaji wa haki za watu wenye ulemavu kwa kuwanyima haki za msingi kama elimu,afya na haki nyingine za kibinadamu.
Amesema rangi ya ngozi waliyonayo watu wenye ualbino siyo ulemavu wa ngozi bali wao wanahesabika katika kundi la watu wenye ulemavu wa macho kutokana hali waliyonayo.
Kwa upande wake mratibu wa wa elimu jumuishi Wilayani Mpanda Bi.Ashura Shabaani ambaye pia ni msichana mwenye ualbino amesema mpaka sasa bado kuna baadhi ya watu wenye ualbino wanaojinyanyapaa.
Amewataka watu wenye ualbino kuchanganyikana na jamii ili kupata elimu inayowawezesha kufahamu haki zao,kupatiwa mafuta ya kupunguza mionzi mikali ya jua.
Watu wenye ualbino Tanzania wamekuwa hawachangamani na jamii wakiogopa mauaji dhidi yao kama ilivyokuwa katika miaka michache iliyopita.

Habari zaidi ni P5TANZANIA LIMITED

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA