MVUA YA LEO MKOANI KATAVI IMELETA MADHARA

Na.Issack Gerald
Mvua zinazoendelea kunyesha mkoani Katavi zimesababisha madhara katika makazi ya wakazi wa Mtaa wa Misunkumilo uliopo Manispaa ya Mpanda ukiwemo uharibifu wa miundombinu.
Baadhi ya wananchi ambao makazi yao yameharibiwa ikiwemo kufa kwa mifugo kutokana na maji kukosa mwelekeo hali inayosababishwa na kutokuwepo kwa mitaro ya maji wameiomba serikali ichukue hatua.
Kwa upande wa Mwenyekiti wa mtaa huo BW Katabi Jona ameutaka uongozi wa Manispaa kuichukulia hatua Kandarasi iliyo husika na ujenzi wa barabara za mtaa huo bila kuweka mitaro.
Haya yana jili ikiwa ni siku moja tu tangu mamlaka ya hali ya hewa nchini TMA kutoa tahadhari juu ya uwepo wa Mvua kubwa.
Habari zaidi ni P5TANZANIA LIMITED


Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA