MBUNGE NASSARI:NIMENUSURIKA KUUWAWA KWA RISASI USIKU

Mbunge wa Jimbo la arumeru Mashariki Joshua Nassari, amevamiwa na watu wasiojulikana nyumbani kwake Usa River mkoani Arusha na kunusurika kupigwa na risasi ambazo zimeua mbwa wake.
Mh.Joshua Nassari
Katika ukurasa wake wa twitter,Nassari ameandika ujumbe akitoa taarifa kuwa watu hao wamevamia nyumbani kwake usiku wakiwa na silaha za moto ambazo wamewafyatulia mbwa wake.
Mbunge huyo mara kadhaa amekuwa akiripoti katika mitandao ya kijamii kuwa amekuwa atishiwa kuuawa mara kwa mara.
Hakuna kauli ya jeshi la polisi ambayo imetolewa kuzungumzia tukio hilo.

Habari zaidi ni P5TANZANIA LIMITED

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA