WAKAZI MPANDA WANAISHI KWA HOFU YA USALAMA, WASHINDWA KUFANYA KAZI

Na.Issack Gerald
Wakazi wa vijiji vya Ndui Stesheni,Mnyaki A na Mnyaki B kata ya Katumba wilayani Mpanda Mkoani Katavi wanashindwa kufanya kazi za maendeleo kwa uhuru kutokana na uharifu unaofanywa na watu wasiojulikana.

Hali hiyo imebainishwa na wakazi wa vijiji hivyo wakati wakizungumza na Mpanda Radio kwa Nyakati tofauti katika vijiji hivyo kutokana na matukio ya watu kuvamiwa nyumbani nyakati za usiku,kutekwa njiani na kuporwa mali.

Wakazi wameliomba jeshi la polisi kuweka mkazo ili kutafuta namna ya kukomesha uharifu huo ambao umekuwa kero kwao.
Mmoja wa viongozi katika maeneo hayo Bw.Hussein Nasri ambaye ni mwenyekiti wa kijiji cha Ndui Stesheni,amekiri kuwepo kwa matukio ya kiuharifu hasa unyang’anyi wa pikipiki matukio ambayo hivi karibuni yameripotiwa na wenyeviti wa vijiji vya Mnyaki A na Mnyaki B.
Hivi karibuni,Kamanda wa Polisi Mkoani Katavi ACP Damas Nyanda,akihojiwa na Mpanda Radio,alitoa kauli kuwa hajapokea za taarifa za kiuharifu za hivi karibuni hali ambayo imeibu maswali mengi miongoni mwa raia kuhusu mawasiliano kati ya kituo cha polisi Katumba na Makao makuu ya Polisi Mkoa.

Habari Zaidi NA P5TANZANIA LIMITED

Comments

Popular posts from this blog

HISTORIA FUPI YA ABDULRAHMAN KINANA ALIYEJUZULU UKATIBU MKUU CCM

FAHAMU HISTORIA YA JOKETI ALIYETUMBULIWA NA UVCCM

HISTORIA FUPI YA LAZARO NYALANDU ALIYEIBWAGA CCM NA KUHAMIA CHADEMA